Wednesday 7 February 2018

TUNDULISSU :""LEMUTUSI :" usirazimishe urafiki sio kuwepo!

Leo nimewaletea sakata la wanasiasa Kati ya TUNDULISSU & LEMUTUSI ...ambalo Bado limasumbua kila kona UKISOMA ALICHOANDIKA #Tundulisu basi Hapan shaka watu hawa wanakanana urafiki Ebu angalia alichosema TUNDULISSU  ðŸ‘‡ðŸ‘‡ðŸ‘‡



LEMUTUZ ASILAZIMISHE URAFIKI USIOKUWEPO!!! .

Leo nimeonyeshwa post iliyopo kwenye Instagram account ya William Malecela aka Lemutuz.

Kwenye post yake, Lemutuz amedai kwamba mimi ni rafiki yake mkubwa na wa miaka mingi, kabla vijana wengi wanaopiga makelele mitandaoni hawajazaliwa.

Lemutuz ameeleza kwamba mwaka 2010 alinipokea Uwanja wa Ndege wa John F. Kennedy, mjini New York, nilipoenda kwenye mahafali ya dada yangu. .

Amewaambia wasomaji wake kwamba alinichukua kwenye gari yake binafsi kutoka JFK hadi Connecticut kwenye graduation ya dada yangu aliyodai ilikuwa Connecticut State University. .

Ili kuthibitisha kauli zake, Lemutuz ameambatanisha picha niliyopiga naye, ambayo nitaielezea shortly. .

Naomba kuweka ukweli wa kauli za Lemutuz wazi ili kuweka rekodi sawa.

Kwanza, nimemfahamu Lemutuz tangu mwezi Mei, 2011. Nilikutana naye mara ya kwanza kwenye mahafali ya mdogo wangu kaka (sio dada) Vincent Mughwai, aliyekuwa anasoma Bridgeport University (sio Connecticut State University). Kama nakumbuka vizuri, Lemutuz alikuwa MC kwenye shughuli hiyo. Na siku hiyo kulikuwa na Watanzania wengine wengi waishio Marekani. .

Lemutuz hakunipokea mimi JFK wala kunipeleka Bridgeport, Connecticut, kwenye gari yake binafsi. Hatukuwa tunafahamiana kabla ya kukutana kwenye graduation ya kaka Vince, siku kadhaa baada ya mimi, mke wangu na ndugu zangu wengine kuwasili Marekani. .

Pili, ni kweli tulipiga picha ambayo ameitoa kama uthibitisho wa 'urafiki' wetu. Siku hiyo, kama ilivyo kwenye shughuli kama hizo, nilipiga picha na Watanzania karibu wote waliohudhuria graduation hiyo.

Hakuishia hapo kwa Habari kamili baki na mimi Hapa hapa RAGBUONE

No comments:

Post a Comment