Friday 27 April 2018

GIGY MONEY AMPA JINA MWANAE MAPEMA


Msanii wa muziki Bongo na video vixen, Gigy Money amejaliwa mtoto wa kike.
Akizungumza na Bongo5 Gigy Money amesema amejifungua usiku wa kuamkia leo April 27, 2018. Hata hivyo Gigy Money amesema mtoto wake haitwii Candy kama ilivyokuwa ikiripotiwa bali anaitwa Mayra.
October mwaka jana katika mahojiano na kipindi cha Uhondo, E FM ndipo Gigy Money aliweka wazi kuhusu mipango yake ya kupata mtoto kwa kueleza, “Watengemee tu mwakani nitakuwa na mtoto Mungu akinisaidia, yaani hiyo ni lazima,”
Gigy Money ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Mimina’ yupo katika mahusiano na mtangazaji wa Choice FM, Mo J

No comments:

Post a Comment