Saturday 17 February 2018

MORINHO :""POGBA... sina ugomvi nae



MOURIHNO HAIKANA BIFU YAKE NA POGBA

Mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho amesema kuwa ripoti kwamba kiungo wa kati wa klabu hiyo anajuta kujiunga na Man United na kwamba huenda angeondoka mwisho wa msimu huu ni za uongo.

Pogba alidaiwa kukasirishwa na hatua ya Mourinho kumchezesha katika safu isio ya mashambulio , lakini Mourinho amesema kuwa hilo sio kweli.
Vilevile amewakosoa wachanganuzi wa soka akisema kuwa sio muhimu kutaja kuhusu mazungumzo yao na wachezaji.

Lakini ameongezea kuwa Pogba anakubali kwamba hajakuwa akicheza vyema.

Alipoulizwa fikira zake kuhusu uvumi huo katika vyombo vya habari, Mourinho alijibu, nadhani una maneno matamu kwa sababu ukisemu uvumi mwingi unafaa kuongezea uongo mwingi.

No comments:

Post a Comment